ADEM Logo

Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu

Stashahada ya Uongozi na Usimamizi wa Elimu (DEMA)

Programu: Stashahada ya Uongozi na Usimamizi wa Elimu (DEMA)
Ada: 850,000/=
Muda: Miaka miwili

MAFUNZO YA STASHAHADA YA UONGOZI NA USIMAMIZI WA ELIMU (DIPLOMA IN EDUCATION MANAGEMENT AND ADMINISTRATION) DEMA

ADEM inawatangazia walimu wote wa Shule za Msingi, Sekondari, Vyuo vya Ualimu, Vyuo vya maendeleo ya Wananchi na Vyuo vya ufundi stadi (VET) kuwa maombi yanapokelewa kwa Mwaka wa Masomo 2022/2023.

WALENGWA WA MAFUNZO

1. Walimu waliopo kazini katika ngazi zote za elimu

2. Viongozi wa elimu katika ngazi ya Shule, Kata Halmashauri na Mkoa.

3. Wathibiti Ubora wa Shule

UTARATIBU WA MAOMBI

Mwombaji anatakiwa kusoma maelekezo na kujaza fomu inayopatikana katika tovuti ya ADEM: www.adem.ac.tz

MUDA WA MAOMBI

Tarehe 01/04/2022 hadi tarehe 30/09/2022

SIFA ZA KUJIUNGA

Mwombaji awe ni mwalimu mwenye uzoefu usiopungua miaka 03 kazini, na ufaulu wa CSEE awe na D nnena katika masomo yasiyo ya dini.

MUDA WA MAFUNZO

Miaka miwili au mihula minne yenye Wiki 15 kila mmoja. Mafunzo yataanza Mwezi Oktoba 2022.

KAMPASI ZA ADEM

Bagamoyo, Mbeya na Mwanza, mwombaji atachagua kituo anachotaka kusomea.

MAWASILIANO

Tuma barua/fomu yako ya maombi kupitia barua pepe: admission@adem.ac.tz AU MTENDAJI MKUU - ADEM S.L.P 71 BAGAMOYO

Kwa maelezo zaidi Wasiliana nasi kwa Simu Na. 0679 649443 ADEM - MWANZA 0786 624 512 ADEM - MBEYA 0765 140487 ADEM - Bagamoyo 0712 690778 ADEM - Vituo vyote