ADEM Logo

Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu

WALIMU WAKUU 50 WILAYA ZA NACHINGWEA, MTAMA, LINDI NA RUANGWA WAFADHILIWA KUSOMA STASHAHADA YA DEMA BURE

01 Mar, 2022
WALIMU WAKUU 50 WILAYA ZA NACHINGWEA, MTAMA, LINDI NA RUANGWA WAFADHILIWA KUSOMA STASHAHADA YA DEMA BURE

Walimu Wakuu na Walimu Wakuu wasaidizi 50 kutoka Wilaya za Nachingwea, Lindi, Ruangwa na Mtama wamepata ufadhili wa kusoma Stashahada ya Uongozi na Usimamizi wa Elimu (DEMA) inayoendeshwa ADEM Bagamoyo.

Programu hiyo inaendeshwa na ADEM kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Aga Khan (AKU) kwa kipindi cha miaka miwili ili kuwajengea uwezo walimu hao katika masuala ya Uongozi na Usimamizi fanisi wa Shule wanazosimamia